This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Monday, February 10, 2014

BANDARI YA DAR ES SALAAM KUFANYAKAZI SAA 24

SERIKALI imesema tatizo la msongamano wa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, utakuwa historia baada ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kuanza kufanyakazi saa 24.


Imesema utaratibu huo utaanza kutumika muda wowote kuanzia sasa na utaongeza tija na ufanisi kwa watumiaji wa bandari.

Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dk. Shaaban Mwinjaka

Hatua ya kuanzisha utaratibu wa kufanyakazi kwa saa 24, imefikiwa na wadau wanaotumia bandari hiyo kwa ajili ya kuongeza huduma bora zinazotolewa na TPA.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka, aliseama hayo jana mjini Dar es Salaam, kwenye hafla ya utiaji saini wa kufanyakazi kwa saa 24 kwa siku saba katika kipindi cha mwaka mmoja baina ya TPA na wadau wengine wa bandari.


Alisema utaratibu huo utapunguza kwa kiasi kikubwa msongamano wa mizigo bandarini na kuongeza ufanisi wa utendajikazi.


“Tunataka kuwahakikishia wananchi kuwa utaratibu huu, utaboresha huduma zinazotolewa na TPA na utaondoa msongamano wa mizigo bandarini,” alisema.

Alisema serikali imeridhishwa na utaratibu huo na itahakikisha unafanikiwa ili kuondoa changamoto zilizokuepo bandarini hapo na kuleta ufanisi kwa watumiaji.
 

Dk. Mwinjaka katika kuhakikisha hilo linafanikiwa, tayari wametenga maeneo kwa ajili ya huduma za kibenki na kwamba nchi zingine wanazofanyanazokazi zitapatiwa maeneo ya ofisi.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPA, Madeni Kipande alisema utaratibu huo utaiwezesha bandari kufanyakazi kwa uhakika na ubora wa hali ya juu.

Friday, February 7, 2014

AIRTEL KUBORESHA MITAMBO YA HUDUMA ZA AIRTEL MONEY WIKENDI HII

· Mabadiliko yataleta ufanisi kwa huduma ya Airtel money
·Mabadiliko yatawezesha  wateja kufanya mambo mengi na kuongeza watumiaji wa huduma ya Airtel money
·  Mabadiliko yataongeza matumizi ya huduma ya Airtel money Tanzania

Dar es Salam, Tanzania 
Airtel Tanzania, kampuni inayoongoza kwa kutoa huduma za kibunifu na zenye ubora nchini iko katika mchakato wa kuboresha mitambo ya huduma ya Airtel money na kuifanya kuwa ya kisasa zaidi.  Mabadiliko haya yatafanyika mwishoni mwa wiki hii  tarehe 7 hadi 9 februari 2014 ambapo baada ya maboresho hayo wateja wa Airtel Money watafurahia ufanisi bora wa mtambo wa Airtel money  wakati wowote watakapotaka kufanya malipo mbalimbali kwa kupitia huduma za kifedha  za simu za mkononi

 Maboresho hayo ya mitambo ya Airtel money wateja wataweza kufanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na  kuunganishwa na huduma mbalimbali na kuongeza ufanisi zaidi . Huduma hii itawawezesha wateja kununua muda wa maongezi, kutuma pesa, na kufanya malipo ya huduma mbalimbali, kutoa na kutuma pesa pamoja na kuongeza huduma mbalimbali wanazotakana kuzitumia kupitia Menu/orodha ya mpya ya huduma hiyo ya Airtel Money zikiwemo zile za kuunganishwa na huduma za kibenki

Akiongea kuhusu mabadiliko hayo ya mitambo, Mkurugenzi wa kitengo cha Mawasiliano Beatrice Singano Mallya (Pichani juu), alisema “kuboreshwa kwa mitambo yetu ya huduma za kifedha ya Airtel money  ni sehemu ya malengo ya Airtel ya kuwawezesha wateja wetu kufanya miamala ya pesa mahali popote wakati wowote kwa urahisi zaidi. Tunaamini maboresho haya yataleta urahisi zaidi kwa watumiaji wa huduma ya Airtel money nchini”

Bi Singano aliendelea kusema, “wakati wa kuboresha hatutegemei kuwa na matatizo yoyote wakati wa zoezi hilo la kuborehsha mitambo yetu na tunawaomba wateja wetu wawe wavumilivu kwa usumbufu utakaojitokeza wakati tutakapokuwa tunafanya zoezi hili kuanzia jumamosi saa 3 usiku hadi jumapili asubuhi . tunawahakikishia wateja wetu wa Airtel Money wote kuwa tunafanya mabadiliko yatakayoleta ufanisi zaidi kwa watumiaji wote,  mashirika binafsi, serikali, mabenki na wadau mbalimbali. Huduma yetu kwa wateja inapatikana masaaa 24 siku zote 7 za wiki ili kuweza kutoa huduma iwapo kutakuwa na matatizo yoyote. Pia tutaweza kuwasaidia wateja wetu watakaowasilisha baadhi ya matatizo kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii yaani Facebook and Twitter.”
Maboresho ya Airtel Money yenye lengo la kuendelea kutoa huduma Bora zaidi pia yanadhihirisha jitihada za Airtel kuendeleza ubunifu wa hali ya juu  kwa kuleta teknolojia mpya za kisasa zaidi katika sekta ya mawasiliano nchini Tanzania, Tumedhamiria kuwaletea wateja wetu huduma bora zaidi inayokwenda sambamba na mahitaji yao ya kila siku. Hii ndio sababu kubwa inayotufanya Airtel kuboresha mtambo wetu wa huduma hii ya Airtel Money kuwa wa kisasa zaidi.

Thursday, February 6, 2014

WASHINDI PROMOSHENI YA MIMI NI BINGWA WAPONGEZA AITEL,

Wakati Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi ya Airtel ikisubiria kuchezesha droo kubwa ya shilingi Milioni 50 kupitia promosheni ya Mimi ni Bingwa, baadhi ya washindi waliokwishapatikana wamejitokeza wakiisifia kampuni hiyo kwa kuratibu promosheni zenye kulenga maendeleo kwa watanzania walio wengi nchini.

Washindi hao wameainisha hayo muda mfupi baada ya kukabidhiwa pesa zao mapema wiki hii kwenye ofisi za makao makuu ya Airtel ziilizopo Morocco jijini Dar es salaam.

Washindi hao wamedai kuwa mara nyingi watu huwa hawaamini promosheni zinazoendeshwa na kampuni ya simu kama Airtel na hivyo kujikuta wakibaki nyuma kwa kuogopa kuthubutu.

“Mi binafsi sikuwahi kumuambia mke wangu kwamba nashiriki kwenye promosheni ya Mimi ni Bingwa sababu huwa akijua nashiriki ananikasirikia na kusema nina matumizi mabaya ya pesa, lakini leo nimeibuka mshindi wa shilingi milioni moja yeye akishuhudia na vilevile nimeshinda tiketi ya kwenda kushuhudia mechi ya Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford,” alisema mshindi huyo Bw. Msemwa Makuzi mkazi wa Dar es salaam.

Mshindi huyo aliendelea kwa kusema, kwa hali ya kawaida ilikuwa ni ngumu kuamini kwamba ameshinda shilingi milioni Moja na tiketi ya kwenda nchini Uingereza kushuhudia mechi ya Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford.

“Kweli mimi kama mtu mwingine yeyote wa kawaida iliniwia vigumu kuamini kwamba nimeibuka mshindi wa pesa hizo na tiketi. Na imenichukua muda kuamini mpaka sasa baada ya kukabidhiwa hizi milioni moja ndo naamini kweli mimi ni mshindi,” alimalizia Bw. Makuzi.

Aidha washindi wengine wamewaasa wananchi kote nchini kujitokeza kwa wingi katika promosheni hiyo kwani ina manufaa makubwa kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa zima.

“Kwa kweli mi nawaambia watanzania wenzangu wasidhani hivi vitu ni masihara, watu wanashinda kweli na maisha yao yanabadilika kupitia hizi pesa tunazopewa. Mimi hapa naiwinda hiyo milioni 50 kwani nina uhakika nikishinda nitakuwa nimesahau kabisa umasikini,” alisema Ramadhani Wefa ambaye ni mshindi wa milioni moja kutoka Kinondoni jijini Dar es salaam.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde alisema bado Airtel inatambua na itaendelea kutambua umuhimu wa wateja wake hivyo haina budi kuhakikisha inatoa huduma bora na zenye manufaa kwa wananchi wote kiujumla.
 “Airtel inaelewa fika kuwa wateja ndio kiini cha maendeleo ya kampuni hiyo na hivyo inajitahidi kuhakikisha inatoa huduma bora za kuwanufaisha wateja wake na kuleta maendeleo kwa taifa zima kiujumla,” alisema Jane.
Afisa Mahusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde (wa pili kushoto) akiongelea umuhimu wa promosheni ya Mimi ni Bingwa muda mfupi baada ya kukabidhi shilingi milioni moja kwa baadhi ya washindi wa promosheni hiyo (waliopo pichani). Kushoto ni Bw. Ramdhani Wefa, Kulia ni Philemon Nathaniel Mgaya akifuatiwa na Bw. Msemwa Makuzi ambaye pia ni mshindi wa tiketi na wote wakiwa wanatokea Dar es salaam.