This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Monday, August 19, 2013

TBL YAZINDUA KAMPENI YA NYUMBANI NI NYUMBANI YA GRAND MATL NA VITA MALT



Meneja mahusiano wa TBL Doris Malulu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya uzinduzi wa kampeni kubwa ya vinywaji hivyo kuwatembelea watumiaji majumbani mwao na kutoa elimu juu ya umuhimu wa kutumia vinywaji vilivyo bora , Kampeni hiyo itajulikana kwa jina la Nyumbani ni Nyumbani na itajumuisha mikoa kumi ya Tanzania Bara,Kulia ni meneja wa vinywaji hivyo Consolata Adam.
Na Mwandishi Wetu
KATIKA kile kinachoonekana kusogeza huduma bora zaidi kwa wananchi na kutambua umuhimu wa afya zao, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia vinywaji vya Grand Malt na Vita Malt imezindua kampeni maalumu iitwayo ‘Nyumbani Ni Nyumbani’ kwa ajili ya kupeleka bidhaa hizo zisizo na kilevi kwa Watanzania wote.

Akizindua kampeni jijini Dar es Salaam jana, Meneja Bidhaa zisizo na vileo wa TBL, Consolata Adam alisema, wamezindua kampeni hiyo maalumu ili kuhakikisha vinywaji visivyo na kilevi vinamfikia kila mtu.

“Tumeamua kuzindua kampeni hii ili kuhakikisha kila Mtanzania anafahamu umuhimu wa vinywaji vya Grandmalt na Vitamalt katika matumizi ya kutunza na kulinda afya zao.

“Kampeni hii itahusisha mabalozi wa Grand Malt na Vita Malt kwa pamoja kutembea nyumba kwa nyumba na kuhakikisha ujumbe huu unamfikia kila mtu katika nyumba yake ambapo pia kutakuwa na fursa ya kujishindia na kuzawadiwa zawadi mbalimbali wakati wa kampeni hiyo,” alisema.

Consolata alisema, vinywaji hivyo ni vizuri zaidi kwa afya ya mwanadamu kwani vimet engenezwa vikiwa na virutubisho vya kila aina na vinafaa mno hata kwa mama mjamzito.

“Tunaomba Watanzania wasishangae pale watakapokutana na watu wetu ambao watakuwa wanawatembelea majumbani kwao, kwani lengo ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya kutambua faida za kutumia kinywaji cha Grand Malt  na Vita Malt katika kulinda afya yake ili tuweze kujenga desturi ya kuwa na matumizi bora kwa ajili ya kujenga afya zetu,” alisema.

Nayee Afisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu alisema hii ni kampeni ya kwanza kuzinduliwa na vinywaji hivyo kwa lengo moja la kuwawezesha Watanzania kutumia bidhaa hizo zenye faida kubwa kwa mwili wa mwanadamu.

“Tunataka bvinywaji hivi vipatikane kila mahali na pia kuwasaidia Watanzania umuhimu wa kuvitumia kwani vina faida kubwa kwa wote, kuanzia hata kwa mtoto,” alisema Doris.

Kampeni hiyo ya ‘Nyumbanio ni Nyumbani’ inatarajiwa kuanza katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Kilimanjaro, Mtwara, Dodoma, Iringa, Morogoro, Mbeya na Shinyanga ambapo itaanzia mji wa Kahama.


Vinywaji vya Grand Malt na Vita Malt ambavyo havina kilevi vinazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

Sunday, August 18, 2013

WABUNGE: SERIKALI ITUMIE RISITI ZA ELEKTONIKI


BY ZITTO KABWE
Major  Highlights
1.) Kutokana na kutokuwepo na taarifa sahihi kuhusu deni la Taifa kuna umuhimu wa kukutanisha wadau wakuu wanaohusika hususani BOT, HAZINA, Kamati za Bunge na CAG ili kuweza kujua kwa usahihi zaidi ukubwa wa deni hilo.  Vile vile imeamuliwa kuwa Serikali ishauriwe kuunda chombo huru kitakachosimamia deni la taifa.
2.) Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma haiweki uwazi wa kutangaza umiliki wa mali za viongozi.  Hii inapelekea viongozi kutoweka wazi mali wanazomiliki na ni rahisi mtu kuzushiwa umiliki usio wa ukweli.  Ni vyema Sekretarieti wakafanya utafiti wa umiliki wa mali kwa viongozi wa Umma na kuweka taarifa hizo katika tovuti ya Sekretariati ili kuwawezesha wananchi kuweza kuona mali zinazomilikiwa na viongozi wao; na pale ambapo kiongozi hatakuwa ametoa taarifa ya umiliki huo basi taarifa hiyo itolewe kwa Tume.
3.) Kwa kuwa leseni za udereva za sasa zinaweza kuweka kumbukumbu za makosa ya usalama barabarani, basi TRA ikishirikiana na  Wizara ya Mambo ya Ndani zihakikishe ya kuwa Askari wa Usalama Barabarani wanatumia utaratibu huu wa kisasa wa kutoa  “notification” na kutoa risiti za malipo za elektroniki.
4.) Maduhuli ya Serikali sasa yakusanywe kwa kutumia risiti za elektroniki.  Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma yaanze kutumia risiti za eletroniki mara moja ili kudhibiti upotevu wa mapato ya serikali yanayotokea hivi sasa katika kutumia risiti zinazoandikwa kwa mkono. Pia ofisi za serikali zifanye manunuzi yake kwa wafanyabiashara wanaotumia mashine za kielektroniki.
5.) “The Proceeds of Crime Act, 1991” ifanyiwe marekebisho na kuweka kifungu kinachomwezesha AG/DPP kuwa na mamlaka ya kuomba mahakama kufungua kesi ya madai (Civil Forfeiture) kwa watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Friday, August 2, 2013

ADV/TANGAZO

MAYFAIR HOTEL

Suites | Conferences | Events

  • Free high-speed wireless Internet Access
  • A Kitchenette with Microwave, Refrigerator, etc.
  • A nice small coffee table with four charis, gives you feel like at home
  • A spacious nice Bathroom with bath tub and hair-dryer, etc.
Contact Details:
Mobile: +255 685-688000
Email: info@mayfairplaza.com
Website: 
www.mayfairhoteltz.com
Address: Mayfair Hotel, Old Bagamoyo Road, Dar es Salaam, Tanzania.

123Tanzania E-Shots
 
27,000+ Subscribers all over the Tanzania.
123Tanzania.com is the largest B2B online directory of Tanzania with more than15,000 monthly visitors

Contact Us: English or Kiswahili +255 773 858 090, +255 22 213 3039

Copyright © 2013 123Tanzania, All rights reserved. 
You are receiving this email from 123tanzania.com, Tanzania's largest Business portal. If you would like to unsubscribe from this list, simply click unsubscribe from the link below. Please note: unsubscribing from this list will only unsubscribe you from Newsletters E-Shots, it will not unsubscribe you from the Promo E-Shots. 

Our mailing address is: 
123Tanzania
Elia Complex
Zanaki Street
Dar Es Salaam 8758
Tanzania

Thursday, August 1, 2013

WAANDISHI WA HABARI WATEMBELEA TBL MBEYA



Waandishi wa habari wa mkoa wa Mbeya wakitembelea kapuni ya Bia TBL
Moja ya watumishi wa kampuni hiyo ya Bia akiwaeleza waandishi wa habari jinsi bia inavyotengenezwa
Ziara inaendelea

Meneja kiwandacha kampuni ya Bia TBL  Mbeya Nicolaus  Kanyamala akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea kiwanda hicho
Baadhi ya wa watumishi wa kampuni ya Bia wakijitambulisha mbele ya waandishi wa habari


Meneja uhusiano wa TBL Dorris Malulu akizungumza na waandishi wa habari
Meneja masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) Kanda ya Mbeya, Raymond  Degera, akielezea mafanikio ya kampuni ya Bia
Mpishi Mkuu wa Bia wa Kampuni ya Tbl, Tito alisema Sheria za Tanzania zinatakiwa kusimamiwa ipasavyo kuhusu matumizi ya Vilevi kwa kuwashtaki wanaozidisha pombe na wengine wanaokunywa mida ya kazi na kuleta usumbufu kwa wengine.
Wanahabari walipata fursa ya kuelezwa sheria za
unywaji wa Pombe na madhara yake, umri wa mtu kuanza kunywa pombe pamoja na
madhara yake ambapo baada ya zoezi hilo walitembelea maeneo mbali mbali ya
Kiwanda hicho.
Baada ya kutembelea kiwanda  sasa ilifika wakati wa kuonja Bia na kuitambua radha yake
Unaonja na kutaja ni bia gani kama ni NDOVU au KILIMANJARO kunaalama za rangi zimewekwa katika grass
Mwandishi wa Mbeya yetu Joseph Mwaisango akionja na kujaza katika fomu kuwa hiyo aliyoinja ni Bia gani
 Meneja
kiwanda cha kampuni ya Bia TBL  Mbeya Nicolaus  Kanyamala akimkabidhi
zawadi Joseph mwaisango mara baada ya kuibuka mshindi wa uwonjaji bia
 Meneja
kiwanda cha kampuni ya Bia TBL  Mbeya Nicolaus  Kanyamala akimkabidhi
zawadi Emmanuel Madafa baada ya kushinda uonjaji wa Bia
Mshindi wa pili Joachim Nyambo akipokea zawadi yake toka kwa meneja wa kampuni ya bia 
Picha ya pamoja



ZAIDI ya Tani 60,000 za Shayiri zinatarajiwa kuvunwa kutoka kwa Wakulima wa  Kanda ya Nyanda za Juu Kusini baada ya kupatiwa mafunzo juu ya kilimo cha mazao yenye tija na uwepo wa soko la uhakika. Aidha zaidi ya Wakulima 400 kutoka Kanda hiyo ndiyo walionufaika na Kilimo hicho na kujihakikishia Soko la zao ambalo hutumika zaidi katika utengenezaji wa Vinywaji moto ambavyo ni Bia na

uzalishaji mwingine kutokana na uwepo wa Viwanda vikubwa vya kuzalisha Vinywaji hivyo.


Hayo yalibainishwa juzi na Meneja masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) Kanda ya Mbeya, Raymond  Degera,wakati wa Ziara ya Waandishi wa Habari katika Kiwanda cha Bia kilichopo Iyunga Jijini Mbeya.


Alisema  kutokana na uwepo wa Kiwanda cha Bia Mkoani Mbeya na kuhudumia Wananchi wa Kanda ya Nyanda za Juu kusini waliona si vema Malighafi zikatoka Nje ya Mikoa hiyo ili hali ardhi na hali ya Hewa inaruhusu kilimo cha mazao hayo na kuamua kutoa elimu namna ya kunufaika na Kilimo.


Degera alisema Kampuni  ilianzisha Programu ya kuwawezesha Wakulima kuhusu kilimo cha mazao yenye tija ambapo Wakulima wa Wilaya ya Mbozi,

Sumbawanga na Iringa wanaofikia 400 ambao waliitikia na kuanza uzalishaji ambao baada ya mavuno kiwanda kitanunua moja kwa moja kutoka kwa wakulima ambao wanatarajia kuvuna Tani 60,000.


Kwa upande wake  Mpishi Mkuu wa Bia wa Kampuni ya Tbl, Tito alisema Sheria za Tanzania zinatakiwa kusimamiwa ipasavyo kuhusu matumizi ya Vilevi kwa kuwashtaki wanaozidisha pombe na wengine wanaokunywa mida ya kazi na kuleta usumbufu kwa wengine.


Alisema Utaratibu wa Nchi zingine huwalazimisha wananchi wake kutumia Chupa mbili za Bia kwa siku na kwamba anayehitaji kuongeza zaidi ya hapo wauzaji huwakatalia, Sheria ambayo alishauri kutumika ili kuongeza uzalishaji na kuiondoa nchi katika majanga yanayotokana na ushawishi wa Pombe.


Aliongeza kuwa  kama wamiliki na watengenezaji wa Pombe wanahitaji wananchi wanywe kwa utaratibu ili waendelee kuwa wateja wao na  kusaidia kuchangia kodi kwa Taifa kutokana na Kampuni hiyo kuongoza kwa kuchangia kodi katika pato la Taifa.


Aidha katika Ziara hiyo Wanahabari walipata fursa ya kuelezwa sheria za unywaji wa Pombe na madhara yake, umri wa mtu kuanza kunywa pombe pamoja na madhara yake ambapo baada ya zoezi hilo walitembelea maeneo mbali mbali ya Kiwanda hicho.


Mbali na hilo wanahabari hao pia walishindanishwa kuonja Bia na kuzitambua kwa majina zoezi ambalo lilikuwa gumu kwa waandishi wengi huku Waandishi wanne wakiibuka washindi baada ya wawili kushika nafasi ya kuanza kwa kupata alama tatu kati ya Tano ambao ni Emmanuel Madafa na Joseph Mwaisango huku alioshika nafasi ya pili kwa kupata alama mbili kwa tano wakiwa ni Joachim Nyambo na Kenneth Ngelesi.