Saturday, December 8, 2012

TANGAZO LA M-PESA YATENGAMAA TENA


Huduma ya M-Pesa ilipata hitilafu jana.
  Kufuatia hitilafu hiyo wahandisi wa mtandao Tanzania wakishirikiaana na wadau wa nchini Uingereza walifanya kazi usiku na mchana ili kutatua tatizo na hatimaye kuwezesha huduma kufanya kazi mida ya jioni.
  Mkurugenzi  wa kitengo cha M-Pesa, Jacques Voogt  amesema  wateja walikua wakipiga  *150*00#   wanapata ujumbe mfupi SMS usemao “Ndugu mteja, huduma ya M-Pesa haipatikani kwa sasa, tafadhali jaribu tena”
  Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza kwa wateja wetu, mawakala wa M-pesa na wadau wetu wote kwa ujumla.
M-Pesa ni huduma pendelevu ya malipo kwa wateja zaidi ya milioni 4.5 na ina wadau wa biashara zaidi ya 200 wanaotumia huduma hii kukusanya na kusambaza pesa.

0 comments:

Post a Comment