Tuesday, December 4, 2012

AIRTEL YAZINDUA PROMOSHENI YA MWISHO WA MWAKA 2012 KWA WATEJA WAKE

* Ni promosheni  ya "AMKA MILIONEA".
* Ndani ya siku 90 wateja 875 wa Airtel kuzoa sh. milion 401


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imezindua promosheni mpya ili kuweza kuwazawadia wateja wake wakati wa msimu huu wa mwisho wa mwaka.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo kwa waandishi wa habari  Meneja wa huduma za ziada wa Airtel Francis Ndikumwami alisema kwamba "Airtel  inakutoa fursa nyingine kwa Tanzania kushiriki na kushinda zawadi ya fedha taslimu wakati wa msimu huu wa sherehe. Leo tunazinduzi "AMKA MILIONEA" amabazo jumla ya zawadi za fedha taslimu zenye thamani ya shilingi milioni 401zitatolewa ndani ya siku 90 tu.

Kutakuwa na washindi wa kila siku, kila wiki, kila mwezi na zawadi kubwa moja itatolewa mwisho wa promosheni, katika promosheni hii wateja wa Airtel 875 watazawadia hizo milioni 401.

AMKA MILIONEA itakuwa na washindi wa aina tofauti tofauti . Washindi wa kila siku, kila wiki na kila mwezi, AMKA MILIONEA itahakikisha kila siku kunawashindi 10 kushinda kila siku na watagawana jumla ya shilingi  3,000.000, kila wiki jumla ya shilingi milioni 6,000,000 zitashindaniwa na washindi 10 na kila  mwisho wa mwezi  mshindi mmoja atashinda kitita cha shilingi milioni 30 wakati milioni  50, 0000 Tshs itaenda kwa mshindi mmoja mwisho wa promosheni hii.

Akizungumza jinsi ya kujiunga na promosheni hiyo  Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema, Ili mteja aweze kushiriki inabidi atume neno WIN/SHINDA kwenda namba 15595 bure na utakuwa ujiungajiunga, Baada kujiunga mteja atakuwa atapata ujumbe kutoka 15656 na kupata maswali ambayo atajibu na akipata sahihi atapata ponti 20 akikosea atapata ponti 10. Na kwakila ujumbe atakaotuma atatozwa kiasi cha shilingi 350 pamoja na kodi.

Amka milionea imeanza leo Desemba 3, 2012 itaenda hadi Machi 2, 2013

Vigezo Muhimu
Mshiriki mmoja hawezi kushinda zaidi ya 1 ya kwa zawad ya kila siku .
Mshiriki mmoja hawezi kushinda zaidi ya 1 yakwa zawadi ya kila wiki
Mshiriki mmoja hawezi kushinda zaidi ya 1 zawadi ya kila mwezi.
Mshiriki mmoja unaweza kushinda mara moja zawadi ya kila siku, mara
moja zawadi ya kila wiki  na mara 1 zawadi ya kila mwezi. Lakini pia
anaweza akajishindia zawadi kubwa ya mwisho wa promosheni

Kujiunga
Tuma neno "WIN / Shinda", kwenda namba 15595 ( bure), na kisha utapokea ujumbe wa ukaribisho utakaombatana na maswali utakayojibu.

Kila jibu sahihi mteja atapata pointi/alama 20 na akikosea atapata pointi 10 zitakazomuwezesha kushinda, ukijibu maswali mengi unajiongezea nafasi ya ushindi

0 comments:

Post a Comment