This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Monday, October 21, 2013

TAKWIMU KUHUSU PATO LA TAIFA



Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Wizara ya Fedha ina jukumu la kukokotoa Pato la Taifa kwa robo Mwaka ili kuwapatia takwimu  kwa wakati, wadau wa takwimu za Pato la Taifa katika vipindi vifupi vya robo mwaka ili kuweza kutathmini mabadiliko ya ukuaji wa uchumi.

Ukuaji halisi wa Pato la Taifa la Tanzania kwa bei za soko uliongezeka kwa kasi ya asilimia 6.7 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2013 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 6.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2012. Jumla ya thamani ya Pato la Taifa katika kipindi husika ilikuwa Shilingi 5,012,935 milioni mwaka 2013 ikilinganishwa na Shilingi 4,699,884 milioni mwaka 2012.

Ukuaji wa Shughuli za Uchumi za Kilimo na Uvuvi
Shughuli za kiuchumi za kilimo zilifikia kasi ya ukuaji ya asilimia 5.3 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2013 zikilinganishwa na asilimia 5.1 ya robo kama hiyo mwaka 2012. Katika kipindi hicho, kulikuwa na mvua za kutosha katika mikoa inayozalisha mazao kwa wingi. Aidha, maelekezo ya ma-ofisa Ugani kwa wakulima kama kuchagua aina bora ya mbegu yalisaidia kuongeza uzalishaji.

Shughuli za uvuvi zilifikia kasi ya ukuaji wa asilimia 2.4 katika robo ya pili ya mwaka 2013 ikilinganishwa na asilimia 6.5 katika kipindi kama hicho mwaka 2012. Kasi ya ukuaji huu ilipugua kutokana na kupungua kwa mavuno ya samaki kutoka kwenye maziwa, mito na mabwawa.

Shughuli za Uchumi za Viwanda na Ujenzi
Shughuli za uchimbaji madini, mawe na kokoto ziliongezeka kwa kasi ya asilimia 4.3 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2013 ikilinganishwa na kuporomoka kwa kasi ya ukuaji wa asilimia 5.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2012. Kuongezeka kwa kasi hii ya ukuaji ilitokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa madini ya almasi na Tanzanite katika robo ya pili ya mwaka 2013.

Shughuli za uzalishaji bidhaa viwandani zilifikia kasi ya ukuaji ya asilimia 5.8 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2013 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 8.2 mwaka 2012. Kupungua kwa kasi ya ukuaji ya asilimia 2.4 (percentage point) kulitokana na kupungua kwa uzalishaji wa sementi, vyakula vilivyosindikwa na nguo.

Uzalishaji wa nishati ya umeme ulifikia kasi ya ukuaji wa asilimia 4.5 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2013 ikilinganishwa na kuporomoka kwa kasi ya ukuaji ya asilimia 1.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2012. Kuongezeka kwa ukuaji wa nishati ya umeme kwa asilimia 5.6 (percentage point) kulitokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa nishati ya umeme unaotokana  na mafuta na gesi.

Ukuaji wa Shughuli za Uchumi za Utoaji Huduma
Shughuli za biashara za jumla na reja reja, ukarabati wa magari na pikipiki na vifaa vingine vya majumbani zilifikia kasi ya ukuaji wa asilimia 5.9 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2013 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 7.0 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2012. Kupungua kwa kasi kwa asilimia 1.1 (percentage point) kulitokana na kupungua kwa bidhaa zilizotengenezwa hapa nchini na zilizoagizwa kutoka nje ya nchi zilizouzwa katika kipindi hicho.  Shughuli za upangishaji nyumba, na shughuli zingine za biashara zilifikia kasi ya ukuaji wa asilimia 6.7.

Shughuli za uchukuzi na mawasiliano zilifikia kasi ya ukuaji wa asilimia 14.8 katika kipindi husika. Shughuli nyingine ni huduma za Hoteli na migahawa zilizofikia kasi ya ukuaji wa asilimia 3.2; Shughuli za uendeshaji Serikali zilifikia kasi ya asilimia 5.0, Elimu asilimia 5.7 na huduma za Afya na shughuli nyinginezo zilifikia kasi ya ukuaji wa asilimia 3.8 katika kipindi hicho.

Imetolewa na:
Morrice  Oyuke
Mkurugenzi wa Takwimu za Kiuchumi
Ofisi ya Taifa ya Takwimu
Dar es Salaam

Kwa mawasiliano zaidi kuhusu Takwimu za Pato la Taifa kwa robo ya pili ya mwaka 2013, wasiliana na  Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwenye anuani zifuatazo:

Mkurugenzi Mkuu,
Ofisi ya Taifa ya Takwimu,
S.L.P. 796, Dar es Salaam.

Simu: +255 22 212 2722/3/4
Nukushi: +255 22 2130852
Barua pepe: dg@nbs.go.tz  Tovuti:www.nbs.go.tz

Monday, October 14, 2013

MAGAUNI NA VIPODOZI KUTOKA MAREKANI VYAWASILI DAR

flyer-to-blogs   Bringing you fashionable designer office wear (calvin klein, Tahari etc) at an affordable price. Everything is 120,000 and 60,000tshs ONLY. Original MAC Lipstick for TSH 50, 000 ONLY Victoria Secret LipGlossy for TSH 25,000 ONLY

Wednesday, October 9, 2013

TPB YATANGAZA WASHINDI DROO YA MWISHO YA SHEREHEKEA MSIMU WA IDDI NA TPB WESTERN UNION

IMG_0159  
Meneja Mkuu Uendeshaji wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Kolimba Tawa (kulia) akimsoma mmoja wa washindi wa shindano la Sherehekea Msimu wa Iddi na TPB Western Union leo jijini Dar es Salaam.
IMG_0134  
Meneja Mkuu Uendeshaji wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Kolimba Tawa (wa pili kulia) akizungumza kwa njia ya simu na mmoja wa washindi wa shindano la Sherehekea Msimu wa Iddi na TPB Western Union leo jijini Dar es Salaam akimjulisha ushindi wake.
IMG_0101  
Mmoja wa vijana maalumu akikabidhi moja ya kuponi baada ya kuitoa kwenye boksi ili kumpata mmoja wa washindi wa shindano la Sherehekea Msimu wa Iddi na TPB Western Union.
IMG_0092  
Mmoja wa vijana maalumu wakichanganya kuponi kwenye boksi kabla ya kuchagua moja wapo ili kumpata mshindi wa shindano la Sherehekea Msimu wa Iddi na TPB Western Union.
Na Joachim Mushi, Dar
  BENKI ya Posta Tanzania (TPB) hatimaye leo imewataja washindi wa droo ya mwisho wa Shindano la Sherehekea Msimu wa Iddi na TPB Western Union lililokuwa likiendeshwa na benki hiyo. Akizungumza katika hafla fupi na wanahabari jijini Dar es Salaam ya kuwataja washindi hao nane, Meneja Mkuu Uendeshaji wa TPB, Kolimba Tawa alisema zoezi hilo ni mwendelezo wa benki hiyo katika kurejesha sehemu ya mapato ya benki kwa wateja wake. Alisema washindi hao nane kwa jumla wamejishindia shilingi milioni 1.5. Akifafanua zaidi alisema mshindi wa kwanza ambaye ni Elias Mwalamala kutoka Dar es Salaam amejishindia sh. 500,000/-, na mshindi wa pili, Nathan Gawangi kutoka Kigoma akijipatia kitita cha sh. 300,000/-, huku mshindi wa tatu Bruno Hindu (Dar es Salaam) akifanikiwa kuibuka na sh. 200,000/-. Alisema washindi wengine watano ambao nao benki hiyo itawazawadia sh. 100,000/- kila mmoja ni pamoja na Miss Farida kutoka Zanzibar, Alfa Mwakalinga wa Dodoma, Mariam Mtungo, Ramadhan Mapuya kutoka pamoja na Fadhili Daud Mbaga wote kutoka Dar es Salaam. Aidha Tawa aliongeza kuwa washindi wote watapigiwa simu na uongozi wa TPB na kuelekezwa namna ya kupata zawadi zao waliojishindia wakiwa ni miongoni mwa wateja waliotuma na kupokea fedha kupitia huduma ya Western Union. *Imeandaliwa na www.thehabari.com